• Twitter
  • Facebook
  • Google+
  • Instagram
  • Youtube

Monday, 24 August 2015

Weusi wamfuata AKA Afrika Kusini kushoot video yao mpya

May mwaka huu rapper wa Afrika Kusini, AKA alitua jijini Dar es Salaam kwa mwaliko wa Diamond Platnumz kwenye Zari All White Party ambapo alitumbuiza pia.
11821119_1609709415949187_1581297285_n
Joh Makini na G-Nako wakiwa na mwenyeji wao, AKA
Weusi walitumia nafasi hiyo kurekodi ngoma waliyomshirikisha rapper huyo. Nahreel ndiye aliyesimamia utayarishaji wake.
11371277_396233057242302_1001090335_n
G-Nako na AKA
Na sasa Joh Makini na G-Nako wamesafiri hadi jijini Johannesburg, Afrika Kusini kwenda kushoot video hiyo.
11925670_903096329737078_1507720401_n
Weusi wakiwa location?
Wawili hao wamekuwa wakishare picha zinazowaonesha wakiwa kwenye maeneo mbalimbali jijini humo wakiwa na AKA. Wameshare pia kipande cha video kinachomuonesha AKA akiwazungusha kwenye mitaa ya jiji hilo.
11925840_896122883788747_1693845601_n
Picha zinaonesha kuwa tayari wameshoot video hiyo na licha ya kutomtaja muongozaji, hakuna shaka kuwa ni Justin Campos, aliyeshoot video ya Nusu Nusu.

Contact

Get in touch with me


Adress/Street

12 Street West Victoria 1234 Australia

Phone number

+(12) 3456 789

Website

www.johnsmith.com