Monday, 24 August 2015
Msanii wa Endless Fame Films, Mirror amesema alimrekodi Nuh Mziwanda wakati akimtongoza bosi wake Wema Sepetu sababu hakupendezwa na kitendo hicho alichokiona kama ni utovu wa nidhamu.
Akizungumza kwenye kipindi cha Friday Night Live cha EATV, Mirror alisema hawezi kufurahi kumuona ‘dogo’ tu akimtongoza bosi wake.
“Mimi sina matatizo na Nuh cha kwanza na sikurekodi kwa nia ya watu wasikilize,” alisema. “Kwa sababu hata tukiongea ukweli Nuh na madam ni vitu viwili tofauti, [Wema] ni boss, mkubwa hata kwangu. Mimi nilikuwa naangalia movies na sikurekodi kwa nia hata kama akija kusikia girlfriend wake ajue Nuh ndio alikuwa anamsumbua madam,” aliongeza.
Mirror akiwa DJ Ommy Crazy na Sam Misago wa EATV
“Sijawahi kusikia mtu mwingine akimtongoza madam, siwezi kufurahi Nuh akimtongoza bosi wangu kwa sababu yeye ni dogo kama mimi, halafu yeye ana mwanamke wake pia.”
May mwaka huu rapper wa Afrika Kusini, AKA alitua jijini Dar es Salaam kwa mwaliko wa Diamond Platnumz kwenye Zari All White Party ambapo alitumbuiza pia.
Joh Makini na G-Nako wakiwa na mwenyeji wao, AKA
Weusi walitumia nafasi hiyo kurekodi ngoma waliyomshirikisha rapper huyo. Nahreel ndiye aliyesimamia utayarishaji wake.
G-Nako na AKA
Na sasa Joh Makini na G-Nako wamesafiri hadi jijini Johannesburg, Afrika Kusini kwenda kushoot video hiyo.
Weusi wakiwa location?
Wawili hao wamekuwa wakishare picha zinazowaonesha wakiwa kwenye maeneo mbalimbali jijini humo wakiwa na AKA. Wameshare pia kipande cha video kinachomuonesha AKA akiwazungusha kwenye mitaa ya jiji hilo.
Picha zinaonesha kuwa tayari wameshoot video hiyo na licha ya kutomtaja muongozaji, hakuna shaka kuwa ni Justin Campos, aliyeshoot video ya Nusu Nusu.
Sunday, 23 August 2015
Klabu ya Chelsea imeipiku Manchester United katika mbio za kumsajili Pedro Rodriguez, 28, aliyekamilisha uhamisho wake kutoka Barcelona kwa ada ya ya pauni mil 21.1 na mkataba wa miaka minne ndani ya Chelsea.
Pedro akiwa na mchezaji mwenzake wa zamani wa Barcelona Cesc Fabregas
Baada ya uhamisho huo kukamilika Pedro aliwajulisha mashabiki kwa tweet ya kuishukuru klabu ya Barcelona na pia akielezea furaha yake ya kujiunga na mabingwa hao watetezi wa ligi kuu nchini Uingereza.
“Naishukuru klabu ya Barcelona pamoja na Chelsea kwa kufanikisha uhamisho huu, ninatazamia kuendelea kushinda vikombe na klabu Chelsea,” alisema Pedro.
Vikombe ambavyo Pedro amewahi kushinda akiwa na klabu ya Barcelona
Pedro akifanya mazoezi na mlinzi wa Chelsea Cesar Azpilicueta kwenye uwanja wa Cobham
Msimu wa tuzo kwa Diamond Platnumz a.k.a baba Tiffah bado unaendelea, ametajwa kuwania ‘African Youth Choice Awards’ AYCA2015 za nchini Nigeria.
Muimbaji huyo wa ‘Nana’ anawania vipengele viwili kwenye tuzo hizo, ambavyo ni YOUTH CHOICE Artiste Of The Year pamoja na YOUTH CHOICE Best Male.
Hivi ni vipengele anavyoshindania:
YOUTH CHOICE Artiste Of The Year:
wizkid – Nigeria
Davido – Nigeria
Yemi Alade – Nigeria
Sarkodie – Ghana
Aka – South Africa
Eddy Kenzo – Uganda
Diamond Platnumz – Tanzania
wizkid – Nigeria
Davido – Nigeria
Yemi Alade – Nigeria
Sarkodie – Ghana
Aka – South Africa
Eddy Kenzo – Uganda
Diamond Platnumz – Tanzania
YOUTH CHOICE Best Male:
Aka – South Africa
Olamide – Nigeria
Stoneboy – Ghana
Skales – Nigeria
Diamond Platnumz – Tanzania
Patorankin – Nigeria
Aka – South Africa
Olamide – Nigeria
Stoneboy – Ghana
Skales – Nigeria
Diamond Platnumz – Tanzania
Patorankin – Nigeria
